Skip to main content

Status: Closed — this petition is no longer accepting signatures.

Msolla ajiuzulu Sasa!

Msolla ajiuzulu Sasa!

Closed — 8 supporters Verified

Final supporters

H
Halifa M.
S
social b.
T
tomdtenv
I
iblbaslnliw
Y
yydvzwh
P
pskiqznn
B
bqerybgmk
?
?
Started by Anonymous 19 years, 3 months ago
Utangulizi: Katika nchi inayojaribu kujenga utawala wa kidemokrasia kwa misingi ya usawa, haki, uwazi, ukweli, uwajibikaji na uwakilishi basi wananchi wanayo kila sababu ya kutaka serikali yao ijue haja na shida zao. Wananchi hao wanaweza kufanya hivyo kwa kupiga kura, kutoa maoni na pia kuisihi serikali kufanya jambo fulani. Katika kufikisha mawazo na maoni yao wananchi wanaweza kuandika, kuandamana, au kutumia njia mbalimbali za kikatiba kuilazimisha serikali yao kufanya jambo fulani au kutofanya jambo fulani. Ni kwa sababu hiyo basi, sisi wananchi wa Tanzania toka kila kona ya dunia, tukiwa na tofauti za rangi, dini, mahali, vyeo, hadhi, elimu n.k tumeamua kukubaliana kuleta ombi hili kwa uongozi wa serikali ya nchi yetu, tukiwa tumeungana na kukubaliana toka moyoni, kwa ajili yetu na kwa ajili ya uzao wetu, tukiwa kando na kutupilia mbali tofauti zetu zote na kukubaliana kuwa: Kwa vile chini ya Uongozi wa Prof. Peter Mahamoud Msolla, Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya juu imeshindwa kuja na sera inayoeleweka juu ya sekta hizo, na hasa sekta ya Elimu ya Juu; Kwa vile chini ya Uongozi wa Prof. Msolla, elimu ya juu imeendelea kukabiliwa na changamoto za migomo na maendeleo na hivyo kuvuruga mchakato mzima wa upatikanaji wa elimu ya juu; Kwa vile chini ya uongozi wa Prof. Msolla matumizi ya vyeti vya kughushi na sifa za kughushi za kitaaluma umekithiri hadi kwenye baraza la mawaziri na Bungeni, bila hatua madhubuti kuchukuliwa; Kwa vile basi, chini ya uongozi wa Prof. Msolla wanafunzi wa elimu ya juu walioko nyumbani na wale walioko nje ya nchi wanakabiliwa na changamoto mbalimbali za kugharimia elimu hiyo huku wizara yake ikishindwa kabisa kutafuta suluhisho la uhakika, la kudumu, na la haki; Kwa vile basi, chini ya uongozi wa Prof. Msolla wanafunzi 29 wa Kitanzania ambao waliondoka nchini wakiwa na imani na ujuzi wote kuwa serikali itawagharimia elimu hiyo na sasa wamejikuta wakiwa ombaomba katika nchi ya ugeni huko Ukraine huku Ofisi ya Msolla ikiwakana, kuwasusa na kuwazira; Kwa vile basi, Prof. Msolla ameshindwa kuisimamia ipasavyo Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya juu na hivyo kuruhusu ukiritimba usio na sababu, na mchakato mbovu wa utoaji wa mikopo hiyo; Kwa vile basi, Prof. Msolla amekuwa na kiburi cha madaraka, uvivu wa uongozi na ugoigoi wa ubunifu wa kutatua matatizo mengi yanayokabili wizara hiyo; Hivyo basi, sisi wananchi wa Tanzania kwa kauli moja isiyo na utata, kigeugeu wala kubadilika, tunamtaka Prof. Msolla awajibike yeye mwenyewe na kujiuzulu wadhifa wake huo, ili Mtanzania mwingine mwenye uwezo wa kuongoza wizara hiyo nyeti apewe nafasi. Kama Prof. Msolla hataki kuwajibika yeye mwenyewe tunamsihi Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete amwajibishe mara moja. Tafadhali, sahihi zenye kutumia lugha ya matusi au vitisho vya madhara zitafutwa. Lengo letu ni kukusanya si chini ya sahihi 500!

Updates

May 24, 2007

I have spent my nights reading through your stories about the state of our education system and each one reminds me why we must demand accountability. While the ministry remains silent on these issues we are building a clear record of our collective frustration that they cannot ignore forever.

May 24, 2007

Seeing this level of support for a future where our education system actually values integrity is overwhelming. My heart is heavy seeing how many of you share this painful frustration with me, but feeling this momentum gives me real hope for change.

3 Comments

S
Sarah Jenkins
19 years ago Featured

Too much corruption and no real direction. The students are suffering while he stays in office. Kazi imemshinda.

H
Hamisi Reeves
19 years ago Featured

Msolla lazima awajibike. Hakuna maendeleo yoyote yamefanyika kwenye elimu ya juu. Tunaomba mabadiliko ya kweli.

J
Juma Pearson
19 years ago Featured

Aondoke tu hatufai kabisa. Elimu yetu inazidi kushuka kila siku wakati yeye yupo tu anatazama. Inatosha sasa.