TUMESIKITISHWA SANA NA UKIMYA WA SERIKALI ZETU
Issa Shivji Dar es Salaam 0

TUMESIKITISHWA SANA NA UKIMYA WA SERIKALI ZETU

82 people have signed this petition. Add your name now!
Issa Shivji Dar es Salaam 0 Comments
82 people have signed. Add your voice!
17%
Maxine K. signed just now
Adam B. signed just now

  1. Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania



Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni

Rais wa Jamhuri ya Uganda



Mheshimiwa William Samoei Arap Ruto

Rais wa Jamhuri ya Kenya



Sisi, wana Afrika Mashariki, tumesikitishwa na kuaibishwa sana na ukimya wa serikali zetu kuhusu mauaji ya kimbari yanayoendelea Gaza. Ni aibu kubwa sana kuona serikali zetu zikishindwa kutoa kauli hata moja kulaani ukatili unaofanywa na Israel dhidi ya watu wa Gaza.



Kwa maksudi kabisa, Israel inawanyima chakula na hata maji ya kunywa watu wa Gaza, wakiwemo watoto na mama wajawazito. Unyama na ukatili wa kiwango hikii haujatokea duniani kwa karibu karne mbili



Lengo la Israel ni kuua wakazi wote wa Gaza, au kuwahamisha kwa mabavu ili walowezi wa kizayuni waimiliki Gaza. Kwa zaidi ya miaka 75 lengo la Israel limekuwa kupanua mipaka yake ili kumeza nchi nzima ya Palestina pamoja na Gaza na West Bank.



Syio tu kwamba serikali zetu zimeshindwa kulaani haya matendo ya Israel, lakini zinazuia wananchi wake hata kuaandamana, au kwa njia nyingine yoyote, kuonyesha mshikamano wao na binadamu wenzao wa Gaza.



Licha ya kuchelewa sana, tunawasihi na kwa matumaini kuwa, serikali zote tatu zitazinduka na kuchukua msimamo ambao serikali yoyote inayojiheshimu na inayojaali ubinadamu inastahili kuchukua.




Share for Success

Comment

82

Signatures

contribute iPetitions
iPetitions is powered by everyday people — not corporations. With nearly 50 million signatures, we've helped spark change in local communities across the globe. We don't take corporate money. We rely on people like you.
Support iPetitions. Help keep us independent and make real change. Help us stay independent. Every dollar helps.
Processed by Paypal and Stripe.
Enter your details on the next page
iPetitions is powered by everyday people — not corporations. With nearly 50 million signatures, we've helped spark change in local communities across the globe. We don't take corporate money. We rely on people like you.