Skip to main content
BUNGE LIVE NOW

BUNGE LIVE NOW

30 signatures 20 to reach 50
K
Kabuzi signed
A
Ahadi signed
A
alex m. signed
A
Amos O. signed
D
Daniel K. signed
W
Wissman b. signed
E
Emmanuel K. signed
A
Allan M. signed
J
Joshua N. signed
S
Someone signed
PM
Started by Paul Mongi 10 years, 3 months ago

TAMKO:
Sisi, raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tunatumia haki yetu ya Kikatiba kutoa maoni yetu, kuhusu kitendo kiovu cha Serikali kuzuia matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama ifuatavyo:

  1. Kwa kuwa, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 18-2, inayosema "Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii",
  2. Kwa kuwa, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 8(1)-a "wananchi ndio msingi wa MAMLAKA YOTE na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujubu wa Katiba hii",
  3. Na kwa kuwa, kwa mujibu wa Katiba hii, "Ibara ya 8(1)-c, Serikali itawajibika kwa wananchi", na "(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii",

Tunatoa tamko lifuatalo:

  1. Serikali imekiuka masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwanyima wananchi haki yao ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali mchini na duniani ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia, juu ya masuala muhimu kwa jamii, HUSUSAN matangazo ya moja kwa moja ya Vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  2. Serikali imetoa kisingizio kwamba gharama za matangazo hayo ni Shilingi za Tanzania Bilioni 4 kwa mwaka, lakini imekataa kupokea michango ya gharama hizo kutoka kwa wananchi, bila kutoa sababu za kuridhisha, hata pale ambapo baadhi ya vyombo vya habari nchini vilipojitolea kubeba gharama hizo moja kwa moja na kutangaza matangazo hayo

Sisi Wananchi, raia wa Tanzania, tumeamua kufanya yafuatayo:

  1. Tutaaacha kununua magazeti yanayochapishwa na vyombo vya habari vinavyosimamiwa na Serikali
  2. Tutaacha kusikiliza vituo vya redio na luninga vinavyoendeshwa na Serikali
  3. Tutafanya hivi kwa kipindi kisichopungua siku 30, baada ya muda usiopungua saa 72, ambazo tunaitaka Serikali iwe imerejesha mfumo wa matangazo ya moja kwa moja kupitia kituo cha luninga cha TBC1, ambacho kinaendeshwa kwa kodi za wananchi, yaani SISI, ambao kwa mujibu wa Katiba "ndio msingi wa MAMLAKA YOTE"!


Serikali yet IMEASI. Imetunyanyasa vya kutosha, imetupuuza vya kutosha, sasa tunasema, hatutanyanyaswa tena na hatutapuuzwa vya kutosha.

HITIMISHO:
Iwapo maendeleo ya kweli yanapaswa kufanyika, ni lazima wananchi wahusishwe! - Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

Updates

May 4, 2016

The government continues to ignore our constitutional right to access parliamentary proceedings. Call your local representative today and demand they push for the restoration of live broadcasts.

May 4, 2016

The momentum behind this demand for transparency proves that the public will not accept being kept in the dark. Call your local representative today and demand they push for the return of live parliamentary coverage.

25 Comments

E
Elimensa Masamu
10 years ago Featured

Ikiwa wananchi hatuwezi kufuatilia mchakato wa bajeti ya taifa, serikali itawezaje kutushirikisha katika utekelezaje wake? Huu ni mwanzo wa serikali kususiwa na wananchi katika mipango yake.

R
Ronald Mushi
10 years ago Featured

Ni haki ya kila Mtanzania kuonyeshwa Shughuli za bunge live ili kujua ni jinsi gani viongozi aliowachagua wanafanya kazi na jinsi gani kodi yake inatumika katika kuleta maendeleo.

T
Thabit Molly
10 years ago Featured

Serikali imetoa kisingizio kwamba gharama za matangazo hayo ni Shilingi za Tanzania Bilioni 4 kwa mwaka, lakini imekataa kupokea michango ya gharama hizo kutoka kwa wananchi, bila kutoa sababu za kuridhisha, hata pale ambapo baadhi ya vyombo vya habari nchini vilipojitolea kubeba gharama hizo moja kwa moja na kutangaza matangazo hayo huu ni ukandamizaji wa haki za raia kwa mujibu wa katika usiopaswa kumbiwa macho.

A
Ahadi
10 years ago

Tunahitaji uhuru wa vyombo vya habari kuzuia Bunge kurushwa live ni ukandamizaji

A
alex mwibaya
10 years ago

Ningependa sana kujua wa wakilishi wetu wanafanya nini, Je? kazi tuliyo watu wanatekeleza? nini mustakabali wa serikali kwa miaka 5 ijayo?

D
Daniel Kindimba
10 years ago

#bunge_live

A
Amos Obeid Mashairi
10 years ago

Tunataka kuona live na tujuwe ni wapi nchi inaharibika kwa makusudi ya baadhi ua viongozi

W
Wissman best
10 years ago

#bunge_live

Help this petition grow

Share it with friends to help reach 50 signatures.

Sign Petition

We never post to your account. Social sign-in is used only to verify your signature.

or sign with Email

Add a comment?

Your signature will be added via . Tell others why you're signing — it's optional.

By signing, you accept iPetitions Terms of Service and Privacy Policy.

Share Petition

Don't stop at signing, share the petition link with friends to multiply our impact

Copy link or share directly

Instagram
QR Code